Friday, March 2, 2012

MKUU WA MKOA  ADAIWA KUKWAMISHA UCHUMI KAGERA






BAADHI ya wananchi wa wilaya za mkoa wa kagera wamedai kukerwa na agizo la mkuu wa mkoa huo Kanal Mstaafu Phabiani Masawe kuwataka kusitisha shughuli zao za kiuchumi kwa saa 4 kila alhamisi ya wiki kwa lengo la kufanya usafi wa mazingira mkoani humo


Hatua hiyo imedaiwa kuwa kikwazo kikubwa cha uchumi kwa wananchi kutokana na muda huo kushindwa kuzalisha mali na kulazimika kujikita katika usafi wa mazingira mbali na kwamba shughuli za usafi hufanyika kila siku kwenye majumba yao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi wananchi hao ambao hawakuwa tayali kuandikwa majina yao, kutoka wilaya za Bukoba,Muleba,Misenyi Karagwe, Ngara,Biharamulo na Chato wameonyesha wasiwasi wao mkubwa katika kupunguza hali ya umaskini mkubwa uliopo hivi sasa iwapo serikali itaendelea na msimamo huo.

Aidha wamedai kukerwa na hatua ya kuzuiwa kufunguliwa kwa maduka ya madawa,Migahawa na huduma za usafiri mpaka kukamilika muda wa kufanya usafi, hatua mabayo inaweza kuongeza madhara makubwa kwa binadamu ikiwa ni pamoja na vifo baada ya wagonjwa kukosa dawa walizoamliwa kununua kwenye maduka hayo.

Hata hivyo wameiomba serikali kuwatumia viongozi wa vitongoji na vijiji katika kukagua usafi kwa kila kaya badala ya kuwataka wananchi kusitisha shughuli zao kwa saa nne pasipo kuzalisha mali ili hali inayoweza kuchangia ongezeko kubwa la umaskini wa vipato.

Jitihada za kumpata mkuu wa mkoa wa kagera Masawe hazikuzaa matunda baada simu zake za mkononi kutopatikana wakati wote alipopigiwa.






No comments:

Post a Comment