Tuesday, November 27, 2012



WATOTO SABA WANUSURIKA KUFA CHATO.



                       Waziri wa ujenzi Dk John Mafufuli akitoa maagizo ya kukamatwa mhudumu wa afya.

Na Daniel Limbe,Chato
WATOTO Saba wamenusurika kuawa kwenye hospitali ya wilaya ya Chato mkoani geita baada ya mhudumu wa afya Maliagoreth Kyaruzi kuwanyofolea maji yenye dawa (drip) wagonjwa waliolazwa kwenye wodi ya watoto kwa madai ya ndugu zao kukataa kufanya usafi wa vyoo vya hospitali hiyo.
 
Watoto walionusurika na vifo hivyo ni Edward Robert(4)mkazi wa kijiji cha Nyamirembe,Kashinje Lukanya(12) mkazi wa Busaka,Iren Nasib(3)mkazi wa Bwanga,Naomi Tumain(5) mkazi wa Kachwamba,Yunis William(3)mkazi wa Kasala,Astelia Siajali(2)mkazi wa Kahumo na Alphonce Makolobelo.
 
Tukio hilo la kusikitisha limetokea leo majira ya saa 2:30 asubuhi baada ya mhudumu huyo wa afya kuwataka ndugu za wagonjwa wote walilazwa kwenye wodi ya wanawake na watoto kwenda kufanya usafi wa vyoo kutokana na kuwepo kwa uchufu unaodaiwa kusababishwa na wagonjwa wenyewe.
 
Wakizungumza na Blog hii baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo William Masai na Ester Misungwi wamesema hatua hiyo ilikuja baada ya ndugu za wagonjwa kukaidi amri iliyotolewa na mhudumu huyo aliyewataka kuondoka ndani ya wodi hizo na kwenda kufanya usafi kwenye vyoo vya hospitali hiyo.
 
Baada ya wananchi hao kukaidi amri hiyo mhudumu huyo anadaiwa alilaejea na kuanza kunyofoa maji yenye dawa yaliyokuwa yamening’iniziwa kwa wagonjwa kwaajili ya matibabu kisha kuondoka ndani ya wodi hiyo huku akiwataka watu walioumizwa na kitendo hicho kushitaki popote watakapo ona panafaa.
 
Hatua hiyo iliwalazimu baadhi ya ndugu za wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo kuutafuta uongozi wa haospitali hiyo kabla ya kuwasiliana na katibu wa mbunge wa jimbo la Chato Gelvas Stephano ambaye naye alizungumza na waziri wa ujenzi ambaye pia ni mbunge wa jimbo hilo ambaye alifika eneo la tukio akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya.
 
Kufuatia hali hiyo Waziri Magufuli alilazimika kuzungumza na wagonjwa,na watumishi wa afya kwa lengo la kusikiliza kero zao muda mchache baada ya kumaliza kujionea hali halisi ya watoto waliokuwa wamenyofolewa drip za dawa kisha kulejeshwa baada ya ndugu za wagonjwa kulalamika.
 
Kutokana na malalamiko mengi yaliyotolewa na wagonjwa kuhusu vitendo vinavyofanywa na mhudumu huyo Waziri Magufuli amelazimika kumwagiza mkuu wa wilaya ya Chato Rodrick Mpogolo kwa kushirikiana na Jeshi la polisi kuhakikisha wanamtafuta na kumkamata mtuhumiwa huyo kisha afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
 
“Bahati nzuri mkuu wa wilaya upo hapa,na Ocd na wewe upo hapa…ninaagiza huyo Maliagoreth akamatwe mara moja na kesho afikishwe mahakamani kujibu tuhuma za kutaka kuuwa wagonjwa saba kwa makusudi”alisema Magufuli
 
“Nasema huyo siyo mhudumu anayetakiwa kufanya kazi ya afya…maana kuwanyofolea drip wagonjwa kwa kosa la ndugu zao kukataa kufanya usafi wa vyoo haliwezi kufumbiwa macho….huyo maliagoreth hafai na ninaomba kuanzia leo asikanyage hapa kwenye hospitali kuja kuhudumia wagonjwa…maana ipo siku hata mimi ataninyofolea drip,naamini mmenielewa”alisema Magufuli na kushangiliwa na wagonjwa.
 
Kadhalika magufuli aliwataka waganga na wauguzi wengine kutoa huduma nzuri kadri ya inavyopaswa na kuwatahadhalisha iwapo watawahudumia wagonjwa vibaya kwa lengo la kulipiza kisasi kwa madai wagonjwa wamewashitaki kwake ambapo amedai kufanya hivyo itakuwa ni kutowatendea haki wagonjwa.
 
Vilevile amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Shaban Ntarambe kuhakikisha anamsimamisha kazi mara moja nesi huyo kwa madai hana sifa za kuendelea kuwa mtumishi kwenye wilaya ya chato.
 
Mkuu wa wilaya ya chato Rodrick Mpogolo mbali na kudai kusikitishwa na tukio hilo ameahidi kuunda tume maalumu itakayochunguza utolewaji wa huduma za afya kwa wananchi wanaofika kutibiwa hapo kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi.
 
Aidha amesema msingi wa serikali ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora na kwamba dosari zinazojitokeza atahakikisha zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu ili kusijitokeza vitendo kama vilivyojitokeza.
 
Kwa upande wake Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya hiyo Dk Pius Buchukundi amekiri  kutokea tukio hilo na kudai kuwa kitendo kilichofanywa na mhudumu wake siyo msimamo wa hospitali bali ni matakwa yake mwenyewe na kwamba atahukumiwa kwa matendo aliyoyatenda yeye mwenyewe.
 
Dk Buchukundi amewataka wagonjwa kutoa ushirikiano kwa uongozi wa hospitali hiyo ili kila kunapojitokeza mapungufu kama hayo yaweze kushughulikiwa haraka badala ya kukaa kimya na kuondoka wakinung’unika.
 
 
 
 

Monday, November 26, 2012


                                             JWTZ LATOA UFAFANUZI MLIPUKO NGARA.


Na Daniel Limbe,Ngara
JESHI la wananchi wa Tanzania  JWTZ  kikosi cha Faru makao makuu ya  Tabora limetoa ufafanuzi juu ya msihndo mkubwa uliojitokeza wilayani ngara mkoani kagera na kusababisha baadhi ya wananchi kuyakimbia kwa muda makazi yao kwa kuhofia maisha kutokana na kile walichodai bomu lilidondoka kwenye kijiji cha Ruganzo wilayani humo.

Katika tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Novemba 22 majira ya saa nane lilisababisha baadhi ya wakazi wa wilaya ya ngara kuishi kwa hofu kubwa kutokana kitu kisichofahamika kudondoka toka angani na kusababisha mshindo mkubwa mithili ya tetemeko la ardhi hali iliyopelekea baadhi ya nyumba kupata nyufa.

Kufuatia hali hiyo kiongozi wa kikosi cha JWTZ  Mnadhimu mkuu wa mafunzo  na utendaji wa kivita Brigedia ya Faru Kanali Simon Lali Hongoa amelazimika kutoa ufafanuzi wa kitu hicho baada ya wataalamu wa mabomu kufika kijiji cha Ruganzo kata ya Kibimba wilayani Ngara na kufanya uchunguzi wa kina baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kushindwa kubaini ni kitu gani pamoja na madhara yake.
Kanali Hongoa alikanusha vikali madai ya wananchi wa ngara kuwa kitu kilichodondoka wilayani humo kilikuwa ni bomu la kivita na kudai kuwa maneno hayo hayakuwa na ukweli wowote kwa kuwa kilichodondoka kilikuwa ni kipande cha setelaiti iliyokuwa ikisafiri angani na inahofiwa kiliishiwa nguvu na kudodoka  katika eneo hilo.

Aidha alidai kuwa uchunguzi wa kitaalamu umebainisha kuwa setelaiti hiyo haina madhara yoyote na wala haikutoka uelekeo wa nchi jirani zinazoendelea na migogoro ya kivita kama baadhi ya maelezo ya wananchi wa wilaya hiyo walivyodai.
Hangoa alisema pamoja na kutokuwepo madhara kila mwananchi anatakiwa kuchukua tahadhari ya kubeba vitu wasivyokuwa na uhakika navyo wakilenga kutaka kupata utajiri wa haraka ambao unaweza kuhatarisha maisha yao na jamii inayowazungukana sanjari na kuleta matatizo kwa taifa.
“Kila inapotokea mtu yeyote akaona kitu ambacho hana uhakika nacho usikichukue kwa masuala ya kupata dili utakuja kufa na kuua familia  ni bora ukatoa taarifa katika vyombo vya usalama”.Alisema Hongoa
 Alitoa mfano wa baadhi ya matukio kama hayo yaliyotokea hivi karibuni ambayo yalisababisha madhara makubwa kwa watoto  wilayani karagwe na Arusha na kusababisha  hasara kwa wazazi wao na hata taifa kwa kupoteza rasilimali watu ambao wangekuwa wazalishaji wa uchumi wa taifa.
Awali kabla  kikosi hicho kutoka Tabora hakijawasili wilayani Ngara kulifika kikosi  cha wataalamu wa kambi ya JWTZ Biharamulo lakini uchunguzi wao ulitia mashaka na kulazimika kutoa taarifa ngazi nyingine kwa ajili ya uchunguzi wa kina licha ya baadhi ya wananchi na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya kibimba kuonyesha utukutu wao kwa kukinyanyua kutoka kilikotua na kukipeleka jirani zaidi na  shule yao zaidi ya mita 500
Kitu hicho kizito kilidondoka usiku wa manane na kuzama nusu yake ardhini kwa ukubwa wa diameta 50 kilomita mbili nje ya uwanja wa ndege wa kijiji cha  Ruganzo ambapo baadhi ya raia  walidhani kuwa ni Kimondo,kilichodondoka na kusababisha mshindo mkubwa uliosikika wilaya nzima na  nchi za jirani.
Akihutubia wananchi Mwenyekiti wa kijiji cha Ruganzo  kata ya kibimba wilaya ya  Ngara mkoani Kagera Salvatori Mbanyi  alisema kuwa kitu hicho kilidondoka kutoka angani na mshindo wake kuwashtua wananchi na asubuhi yake kilionwa na watu karibu na mto Ruvubu unaopita kijiji humo kutoka mpakani mwa nchi ya Burundi kuelekea Rusumo mpakani mwa Ngara na Rwanda.
Mbanyi alisema kuwa mara baada ya wananchi kuona kilichosababisha mlipuko viongozi walipeleka taarifa kwa  jeshi la polisi pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya kwa ajili ya kupata maelekezo na ufafanuzi zaidi  ambapo kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ilianza kazi yake .
Alisema kadri masaa yalivyosogea asubuhi umbo lake liliongezeka na kutanuka kama vile kinataka kulipuka na baadaye hali hiyo iliisha na  baadhi ya wananchi  walianza kukisogelea na kukigusa  kisha  kujaribu kukihamisha huku  watoto na wanafunzi wakikinyofoa nyuzi zilizokifunika                                                                         
                                            Taswira ya setelaiti iliyodondoka wilayani ngara.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Ngara Costantine Kanyasu alisema kutokana na kitu hicho kuanguka eneo la wilaya yake lilisababisha taharuki kubwa kwa wananchi ambapo baadhi yao waliamini kuwa ni kombora la masafa marefu lililorushwa kutoka kutokana na vita vinavyoendelea kwenye nchi ya DRC dhidi ya waasi wa 23 na majeshi la serikali.

Kamanda wa polisi mkoani kagera Philip Karangi aliwataka wananchi wa ngara kushilikiana na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani humo kwa kutoa taarifa za kiusalama mapema ili kuondoa madhara yanayoweza kujitokeza badala ya baadhi ya wananchi kufanya kazi za kitaalamu zisizowahusu hali inayoweza kusababisha madhara makubwa kutokana na uzembe.

Kikosi cha Brigedia ya Faru Makao makuu ya Tabora kinasimamia mikoa minane ya Kanda ya ziwa ikiwa ni Tabora,Shinyanga,Simiyu,Mara,Mwanza,Geita,Kagera na Kigoma.
                                                                          Mwisho.

Sunday, November 11, 2012

                             Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya geita wakiwa katika kikao cha baraza.

Na Daniel Limbe,Geita
WIKI moja baada ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita mkoani hapa kumkataa Daktari wa mifugo Thobias Kiputo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuwadharau na kufunga minada ya mifugo wilayani humo kwa madai ya kuwepo ugonjwa wa miguu na midomo kwa lengo la kuikosesha halmashauri mapato,madiwani hao wameendelea kuonyesha msimamo wao na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kumwondoa wilayani humo.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya geita Charles Kimaro wakati akiwasilisha taarifa ya ugawanywaji wa watumishi na mali za halmashauri ya geita kwa lengo la kuzitenganisha halmashauri tatu kiutawala kutokana na serikali kuanzisha halmashauri ya mji wa geita na halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale.
 
Baada ya Kimaro kuwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha baraza la madiweani kilichoketi leo ili kuivunja halmashauri ya geita na kuanzisha rasmi halmashauri ya mji wa geita na halmashauri za wilaya ya Nyang’hwale na Geita ambapo pamoja na mambo mengine baadhi ya madiwani walionyesha kutaharuki kutokana na kuendelea kulisikia jina la Dk Kiputo.
 
Akichangia hoja ya ugawanaji wa watumishi,mali na madeni ya halmashauri ya wilaya ya geita Diwani wa kata ya Nzera Joseph Musukuma alisema kitendo cha kuendelea kusikia jina la Daktari huyo ndani ya orodha ya watumishi wa halmashauri ni kutowatendea haki kwa kuwa tayari walikwisha azimia kuondolewa kwa mtumishi huyo ndani ya wilaya ya geita.
 
“Mheshimiwa mwenyekiti ninasikitika sana kuendelea kumsikia huyo daktari akiwa kwenye idadi ya watumishi wa halmashauri yetu…tulisha mkataa na kamwe hatumtaki kwenye wilaya yetu…kama ni taratibu za kisheria zifanyike lakini akiwa nje ya wilaya hii… kama hakuna pakumpeleka mrudisheni alikotoka kabla ya kuja wilayani kwetu”alisema Musukuma kwa jazba kali.
 
Kauli hiyo ilisababisha takribani madiwani watatu kuchangia hoja hiyo huku wote wakionyesha msisitizo kuondolewa kabisa jina Daktari huyo huku wakidai kuendelea kulisikia jina hilo nikuwadhihaki madiwani hao kwa kuwa tayari walisha mkabidhi jukumu la kumfukuza kwenye halmashauri yao .
 
Kutokana na hali hiyo gazeti hili lililazimika kumtafuta Daktari huyo amnbapo alipuuza uamuzi huo na kulazimika kuelezea sababu za baadhi ya madiwani hao kumkataa kuendela kufanya kazi kwenye halmashauri hiyo kutokana na alichokisema kuwa baadhi yao wanamiliki zabuni za kukusanya ushuru kwenye minada aliyoifunga kisheria baada ya kuwepo ugonjwa wa miguu na midomo.
 
Aidha alifafanua kuwa pamoja na kumtuhumu kwa sababu mbalimbali baadhi ya madiwani hao wanamiliki maduka ya kuuza pembejeo za kilimo na mifugo licha ya kuwa hawana utalaamu wa kutoa huduma hiyo mhimu hali ambayo imeonekana kuwapunguzia mapato.

“Lakini suala la kufunga minada ya mifugo ni la kitaalamu zaidi…na taratibu za kufunga minada hiyo ilizingatia sheria taratibu na kanuni…na ifahamike kuwa hayo hayakuwa maamuzi yangu binafsi isipokuwa ni agizo la wizara husika ambayo iliazimia kuwekwa karantini ya kuchanja mifugo wote waliopo geita ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo usilete madhara kwa binadamu.
 
Hivi karibuni ikiwani Novemba 1 mwaka huu baraza la madiwani wa halmashauri hiyo liliazimia kuondolewa kwa daktari huyo kwa madai ya utendaji kazi wake kutokuwa na kulidhisha,kujibu jeuri kwa viongozi wenzake pamoja na madiwani hao huku wakimtuhumu kumiliki kampuni ya kutoa chanjo ya mifugo kwa maslahi yake binafsi.
                                                  ELIMU YA AWALI CHATO INATIA AIBU.

Baadhi ya watoto wa shule ya awali katika shule ya msingi Kalema wakiwa wanaendelea na masomo kama walivyokutwa na mmiliki wa blog hii.