Sunday, November 11, 2012

                             Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya geita wakiwa katika kikao cha baraza.

Na Daniel Limbe,Geita
WIKI moja baada ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita mkoani hapa kumkataa Daktari wa mifugo Thobias Kiputo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuwadharau na kufunga minada ya mifugo wilayani humo kwa madai ya kuwepo ugonjwa wa miguu na midomo kwa lengo la kuikosesha halmashauri mapato,madiwani hao wameendelea kuonyesha msimamo wao na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kumwondoa wilayani humo.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya geita Charles Kimaro wakati akiwasilisha taarifa ya ugawanywaji wa watumishi na mali za halmashauri ya geita kwa lengo la kuzitenganisha halmashauri tatu kiutawala kutokana na serikali kuanzisha halmashauri ya mji wa geita na halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale.
 
Baada ya Kimaro kuwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha baraza la madiweani kilichoketi leo ili kuivunja halmashauri ya geita na kuanzisha rasmi halmashauri ya mji wa geita na halmashauri za wilaya ya Nyang’hwale na Geita ambapo pamoja na mambo mengine baadhi ya madiwani walionyesha kutaharuki kutokana na kuendelea kulisikia jina la Dk Kiputo.
 
Akichangia hoja ya ugawanaji wa watumishi,mali na madeni ya halmashauri ya wilaya ya geita Diwani wa kata ya Nzera Joseph Musukuma alisema kitendo cha kuendelea kusikia jina la Daktari huyo ndani ya orodha ya watumishi wa halmashauri ni kutowatendea haki kwa kuwa tayari walikwisha azimia kuondolewa kwa mtumishi huyo ndani ya wilaya ya geita.
 
“Mheshimiwa mwenyekiti ninasikitika sana kuendelea kumsikia huyo daktari akiwa kwenye idadi ya watumishi wa halmashauri yetu…tulisha mkataa na kamwe hatumtaki kwenye wilaya yetu…kama ni taratibu za kisheria zifanyike lakini akiwa nje ya wilaya hii… kama hakuna pakumpeleka mrudisheni alikotoka kabla ya kuja wilayani kwetu”alisema Musukuma kwa jazba kali.
 
Kauli hiyo ilisababisha takribani madiwani watatu kuchangia hoja hiyo huku wote wakionyesha msisitizo kuondolewa kabisa jina Daktari huyo huku wakidai kuendelea kulisikia jina hilo nikuwadhihaki madiwani hao kwa kuwa tayari walisha mkabidhi jukumu la kumfukuza kwenye halmashauri yao .
 
Kutokana na hali hiyo gazeti hili lililazimika kumtafuta Daktari huyo amnbapo alipuuza uamuzi huo na kulazimika kuelezea sababu za baadhi ya madiwani hao kumkataa kuendela kufanya kazi kwenye halmashauri hiyo kutokana na alichokisema kuwa baadhi yao wanamiliki zabuni za kukusanya ushuru kwenye minada aliyoifunga kisheria baada ya kuwepo ugonjwa wa miguu na midomo.
 
Aidha alifafanua kuwa pamoja na kumtuhumu kwa sababu mbalimbali baadhi ya madiwani hao wanamiliki maduka ya kuuza pembejeo za kilimo na mifugo licha ya kuwa hawana utalaamu wa kutoa huduma hiyo mhimu hali ambayo imeonekana kuwapunguzia mapato.

“Lakini suala la kufunga minada ya mifugo ni la kitaalamu zaidi…na taratibu za kufunga minada hiyo ilizingatia sheria taratibu na kanuni…na ifahamike kuwa hayo hayakuwa maamuzi yangu binafsi isipokuwa ni agizo la wizara husika ambayo iliazimia kuwekwa karantini ya kuchanja mifugo wote waliopo geita ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo usilete madhara kwa binadamu.
 
Hivi karibuni ikiwani Novemba 1 mwaka huu baraza la madiwani wa halmashauri hiyo liliazimia kuondolewa kwa daktari huyo kwa madai ya utendaji kazi wake kutokuwa na kulidhisha,kujibu jeuri kwa viongozi wenzake pamoja na madiwani hao huku wakimtuhumu kumiliki kampuni ya kutoa chanjo ya mifugo kwa maslahi yake binafsi.

No comments:

Post a Comment