Wednesday, June 6, 2012


                                              .MAUAJI YA KINYAMA MGODINI GEITA
                                             .MWANAFUNZI WA DARASA LA SIT AUAWA KWA RISASI
                                             .ALIKUWA AKIOKOTA VYUMA CHAKAVU



                                                      Mgodi wa Dhabu wa Geita (GGM)

Na Daniel Limbe, Geita
KWA mara nyingine mgodi wa dhahabu wa Geita[GGM]umeingia katika kashifa kubwa baada ya walinzi wake kumpiga risasi na kumuuwa mtu mmoja ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi kivukoni huku mwingine akijeruhiwa kwa risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.
Tukio la mtoto huyo kupigwa risasi na kufa limepelekea zaidi ya wakazi 800 wa kitongoji cha Mwatulole katika Mji wa Geita Mkoani Geita kufanya maandamano makubwa hadi katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Geita,wakipinga kitendo cha Walinzi wa Mgodi wa Geita kumuua kijana huyo ambaye ni mwananchi mwenzao aliyetambuliwa kwa jina la Hoja Juma..
Maandamanao hayo yalianza jana majira ya saa 5 asubuhi katika kitongoji hicho kilichopo umbali wa kilkomita tatu kutoka katikati ya Mji wa Geita,na kupitia barabara kuu iendayo katika mikoa ya Kagera,Kigoma na Nje ya nchi,na kisha kupita katika eneo la mamlaka ya mji Mdogo hadi katika ofisi ya Mkuu wa wilaya.
Hata hivyo waandamanaji hao hawakufanya vurugu ya aina yoyote kama ambavyo ilitokea hivi karibuni,na baada ya kufika katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Geita waliketi chini na kutaka kuonana na Mkuu huyo wa wilaya.
Walidai kuwa walinzi wa Mgodi wa Geita wamemuua kwa kumpiga kwa risasi mwananchi mwenzao ambaye ni Mwanafunzi wa Darasa la sita katika shule ya Msingi Kivukoni,ambaye pamoja na wenzake waliingia katika eneo la mgodi huo kwa ajili ya kuiba vyuma chakavu na kuviuza ili kupata fedha za kununulia sare za shule.
Bw.Thomas Ngusa ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya shule alipokuwa akisomea marehemu akizungumza katika eneo la maandamano,alisema wamechoshwa na vitendo vya ndugu zao kuuawa ama kujeruhiwa na kusababishiwa vilema vya maisha na walinzi wa mgodi huo,hivyo ni vyema serikali ikachukua hatua za haraka za kudhibiti vitendo hivyo badala ya kuweka nta masikioni kama ilivyo sasa.
“Kwanza tuinataka kujua nini hatima kwa huyu marehemu ambaye tayari ameuawa na yuko kwenye chumba cha kluhifadhia maiti,wao tayari wamemuua na wamekaa kimya sisi ndiyo kwa sasa tunahangaika wamekaa kimya,kwanza hii ni dharau inaonekena hawa wawekezaji wamekwishatudharau sana sisi wanageita na watanzania kwa ujumla…….’’alisema Ngusa na Kuongeza.
“Hiyo ni mojan lakini pili tunataka kujua ni kwa nini sasa mauaji dhidi ya raia wenzetui ndani ya mgodi wa Geita yanaonekana kuzoeleka kwa kiasi kikubwa?!!,nanyi kama serikali mumeweka nta masikioni hivi inamaana hakuna serikali hapa,tunatambua kwamba Maiti siku zote hainja haki lakini mnadhanai inaleta picha gani kwa jamii na hasa ndugu,huu ndio tunaita uhasama na kwamba kama serikali haitachukua hatua za haraka katika kutatau tatizo hili ni wazi kwamba kuna siku nchi hii itakuja kutikisika…..’’.
Kwa mujibu wa habari zilkizothibitishwa na jeshi la polisi wilayani Geita Marehemu amefariki Dunia baada ya kupigwa risasi kwenye ubavu wa kulia huku mmwenzake mmoja aliyetambuliwa kwa jina la SwiraMussa (18),ambaye pamoja na majeraha ya risasi aliyo nayo mwilini anashikiliwa na jeshi la Polisi katika kituo kikuu cha polisi Mjini hapa.
Mkuu wa Polisi wa wilaya ya Geita Ronard Makona alithibitishia Gazeti hili kutokea kwan tukio hilo pamoja na kuwepo kwa maandamano ya wananchi hao,huku akimtaja Mlinzi wa Mgodi wa Geita anayedaiwa kumuu kwa risais mwanafunzi huyo kuwa ni Exavery Revocatus ambaye anafanya kazi ya ulinzi katika kampuni ya G4S iliyoko katika Mgodi wa Geita ambaye anashikiliwa na polisi Mjini Geita.
Akizungumzia tukio hilo Baba Mzazi wa Marehemu Leonard Salala alisema amesikitishwa na mauaji ya mwanaye yaliyofanywa na walinzi hao wa mgodi wa Geita,na kwamba hakutegemea kama angepatwa na kifo kwa wakati huu kwani alikuwa amemuacha nyumbani na kwenda kutafuta fedha za kumnunulia sare za shule baada ya kufukuzwa shuleni.
“Alifukuzwa shule kwa sababu hakuwa na sare na ni kweli kwa sababu maisha tunayoishi ni magumu na hasa ikizingatiwa kwamba naishi naye peke yangu baada ya Mke wangu kukimbia kutokana na maisha yetu kuwa ya dhiki,na hiyo siku(Jana)..nilimuacha nyumbani na kumwambia nakwenda kutafuta fedha ili nikamnunulie sare……’’ alisema Baba wa Marehemu.
Aliongeza…”Niliporudi nikapata taarifa kwamba alifuatwa na vijana wenzake na kuwambia kwamba waende huko mgodi wakachukue vyuma chakavu ili wauze na kwa sababu wenzake wamekuwa wakifanya biashara hiyo alishawishika na kuamua kwenda na ndipo alipokutwa na kifo hicho…..’’.
Kwa mujibu wa taarifa ya Daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Dk.Venance Nyanda,kifo cha marehemu kimesababishwa na Kuvuja damu nyingi iliyotokana na kupigwea risasi kwenye ubavu wa kulia na hivyo kuharibu vibaya mapafu yake.
Hili ni tukio la tatu kutokea katika kipindi cha kisichozidi miezi miwili ambapo katika matukio mengine kama hilo wananchi wa mji wa Geita waliandamana na kufanya vurugu kubwa ikiwa ni pamoja na kuchoma moto magari ya Mgodi huo.
Akizungumza na wananchi hao waliondamana katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo aliyeko Safarini Mjini Dodoma Katibu Tawala Wa Wilaya Moses Minga,aliwataka wananchi hao kuacha vitisho kwa wafanyakazi wa Mgodi huo,pamoja na kuwanyang’anya silahan walinzi wa mgodi huo.
Kauli hiyo ya Katibu Tawala ilikuja kutokana na wananchi hao kukataa kuuchukuwa mwili wa marehemu katika chumba cha kuhifadhia maiti,huku wakiwapiga marufuku wafanyakazi wa mgodi huo kuishi nao mitaani bali wakaishi ndani ya mgodi kwa vile wamegeuka wauaji wa kuwaua ndugu zao bila kujali utu wa Mwanadamu.
Aidha wananchi hao waliutupia lawama uongozi wa wilaya kwa kutojali na kushughulikia mauaji ya ndugu zao ambao wamedai wamekuwa wakiuawa mara kwa mara katika eneo la Mgodi huo na,huku wakisistiza kwamba unapopita pembezoni mwa mgodi huo unakutana na harufu wanazodaiwa ni za watu waliouawa na walinzi wa mgodi huo.
Hata hivyo kauli hiyo ilipingwa vikali na Katibu Tawala huyo wa wilaya na kueleza kwamba serikali imekuwa ikifanyia kazi malalamiko mbalimbali yanayotolewa juu ya mauaji yanayodaiwa kufanyika ndani ya mgodi huo dhidi ya raia,na kuwaonya wananchi hao kuacha vitisho dhidi ya wafanyakazi wa mgodi wa GGM pamoja na wawekezaji.

No comments:

Post a Comment