Friday, June 22, 2012

                                             AGIZO LA MKUU WA MKOA LAPUUZWA




                                            Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo

Na Daniel Limbe,Geita
SIKU chache baada ya mkuu wa mkoa wa mwanza injinia Evarist Ndikilo kutoa siku saba kwa baadhi ya viongozi wa idara ya misitu wilayani geita mkoa wa mwanza kuchukuliwa sheria kali kutokana na tuhuma za ubadhilifu na utendaji kazi mbovu,agizo hilo limeonekana kugonga mwamba.

Katika agizo lake mkuu wa mkoa huo alimtaka mkurugenzi wa halmashauri ya geita Mpangalukera Tatala kuhakikisha watendaji waliochini ya ofisi yake (Misitu) ambao wamebainika na tuhuma za kuhujumu raslimali za nchi kutokana na maslahi yao binafsi wanachukuliwa sheria kali pasipo kujali nyadhifa walizonazo.

Agizo hilo alilitoa hivi karibuni kwenye kikao cha wakuu wa idara wa halmashauri hiyo huku akiomba kupewa taarifa za utekelezaji wa agizo hilo kabla ya februali 29 ambapo uchunguzi wa gazeti hili umebaini agizo halijatekelezwa.

Waliotuhumiwa kuhusika na utendaji kazi mbovu wenye lengo la kujinufaisha kinyume cha sheria ni Charles Tui na Emmanuel Marekano ambao walidaiwa kujihusisha na shughuli za ukamataji wa mazao ya misitu polini kisha kuyauza kwa watu binafsi pasipo kuzingatia kanuni na taratibu za kiutumishi.

Ndikilo alidai uchunguzi alioufanya katika ziara yake wilayani humo ulibaini watumishi hao kufanya kazi kwa mazoea kinyume na maadili ya utumishi wa umma kitendo alichodai hakiwezi kufumbiwa macho na serikali.

“Ninasema kwa utendaji kazi wa namna hii kamwe serikali haiwezi kuwafumbia macho watendaji wenye kufanya kazi kwa mazoea kwa lengo la wao kujinufaisha huku wakijua wazi kufanya hivyo ni kosa kisheria”alisema Ndikilo

Hata hivyo gazeti hili liliazimika kumtafuta mkurugenzi wa halmashauri ya geita kwa lengo la kupata ufafanuzi wa agizo la mkuu wa mkoa alililolitoa hivi karibuni,ambapo jitihada hizo ziligonga mwamba baada ya simu zake za mkononui kutopatikana

No comments:

Post a Comment