Wednesday, June 6, 2012

                              CHADEMA YAMKOMALIA NGEREJA NA WENZAKE


                                         Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willbroad Slaa.
Na. Daniel Limbe,Sengerema
CHAMA cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kimesema lazima kiwafikishe kwenye vyombo vya sheria aliyekuwa waziri wa nishati na madini Wiliam Ngeleja na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema Mathew Lubongeja kwa kosa la kushindwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusababisha ufisadi wa mamilioni ya fedha za serikali kwenye halmashauri hiyo.
 
Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya waziri mkuu Mizengo Pinda kutoa agizo la kuhakikisha wakurugenzi wa halmashauri za wilaya ya Sengerema na Misungwi mkoani Mwanza wanachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwafikisha mahakamani kwa kosa na ulaji wa fedha za umma kwa mujibu wa taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali [CAG] ya mwaka 2009/10.
 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya CAG ni kwamba watumishi 21 katika halmashauri ya Sengerema wa idara za fedha,manunuzi,elimu,maji,ujenzi,afya na kilimo na mifugo wametajwa kuhusika kutafuna sh.2.5 bill fedha za miradi ya maendeleo hatua ambayo mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo mei 8,mwaka huu alimlazimu kutoa siku 14 kwa watumishi hao kuandika barua za kujitetea juu ya tuhuma zinazowakabili.
 
Kufuatia hatua hiyo chadema kimedai hakiwezi kukaa kimiya kwa kulifumbia macho sakata hilo na kusema kuwa serikali inapaswa kuwafikisha makamani haraka kabla ya chama hicho hakijachukua uamuzi mgumu wa kuwapandisha mahakamani  kwa nguvu watuhumiwa hao akiwemo mwenyekiti Lubongeja aliyesaini mikata hewa na kujirimbikizia mali .
 
Katika kutekeleza hatua hiyo waliokuwa madiwani wa ccm kata za Nyampulukano Hamisi Tabasamu na Adrian Tizeba kata ya Lugata baada ya kuhamia chadema wamesema wako tayari kwenda kutoa ushahidi mahakamani kuhusu namna fedha hizo zilivyoliwa kutokana na mwenyekiti kushindwa kusimamia vyema majukumu yake.
 
Kauli ya kuwaburuza mahakamani Ngeleja na Lubongeja ilitolewa juzi kwa nyakati tofauti na mbunge wa jimbo la Nyamagana[chadema]Ezekiel Wenje wakati akiwahutubia wananchi wa Katunguru kwenye kata ya mwenyekiti huyo na Sengerema,huku akilaani kitendo cha Ngeleja kujisafisha kwa kutumia mabango ya magazeti yaliyochapisha taarifa ya kichwa cha habari Zitto Kabwe amsafisha Ngeleja.
 
‘’Zitto hata siku moja hawezi kumsafisha Ngeleja…amsafishe wakati yeye ndiyo alikuwa anakusanya sahihi za kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa kushindwa kuwasimamia mawaziri wake,hili Gazeti[jina linahifadhiwa]ni ccm na haitatokea Zitto akafanya kitendo hicho’’alisema mbunge huyo.
 
Wenje alisema mwenyekiti wa halmashauri ya Sengerema  kati ya mikataba 73 aliyoisaini ,mikataba 13 ni mikataba hewa suala ambalo alisema sio la kulifumbia macho huku akikemea wananchi kujichukulia sheria mikononi za kuwapiga na kuwauwa wezi wa mifugo na mali zingine na badala yake wajikite kufuatilia waliokula fedha za serikali ndiyo wanaotakiwa kufanyiwa kitendo hicho.
 
‘’Lazima huyu[mwenyekiti]tumshitaki na kama itashindikana tutafanya maandamano ya amani kushinikiza serikali iwafikishe kortini,naye mbunge wenu[Ngeleja]kutokana na kashifa ya ufisadi wa sh.600 mill lazima tupande naye mahakamani..acheni ajisafishe’’alisema Wenje.
 
Kwa upande wake aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema aliwataka wananchi kutambua uthamani wa maisha yao kupinga unyanyasaji na kutoa wito kushikamana katika kupinga hali hiyo ambayo baadhi ya watu wamekuwa wakiundiwa kesi na polisi kwa kuwabambikiziwa kesi za mauaji,ubakaji na kuwapeleka magerezaji kwa kupinga kauliza viongozi wa vyama vya siasa na serikali.
 
Katika hatua nyingine,Lema alisema kama serikali itashindwa kuwafikisha mahakamani mawaziri walioondolewa katika nafasi zao akiwemo mbunge wa jimbo la Sengerema Ngeleja kwa ufisadi inapaswa wafungwa walioko magerezani kwa makosa ya wizi wa simu,ng’ombe,kuku na baiskeli wafunguliwe wawe huru.
 
Aidha chama hicho kilivuna wanachama wa ccm 20,waliorudisha kadi zao na kujiunga na chadema kutoka Katunguru na Sengerema mjini,muda mfupi baada ya Lema kutangaza oporesheni ya nchi nzima ya”Vua Ngamba Vaa Gwanda’’

No comments:

Post a Comment