Wednesday, June 6, 2012


                       .SERIKALI YAWAONYA WAUZAJI WA DAWA ZA BINADAMU



                                        Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii Dk Haji Mponda

Na Daniel Limbe,Chato
SERIKALI kupitia mamlaka ya chakula na dawa nchini imeonya vikali vitendo vya baadhi ya wauzaji wa maduka ya dawa baridi za binadamu kuendesha shughuli za kitabibu kwenye maduka yao kinyume cha sheria na kwamba huduma hizo zinapaswa kutolewa kwenye Hospitali,vituo vya afya na zahanati zilizosajiriwa kisheria.
Kwa mujibu wa uchunguzi  uliofanywa na wizara ya afya  kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Management Sciences for Health (MSH) mwezi aprili hadi mei 2001 walibaini ukiukwaji mkubwa wa utoaji huduma kwenye maduka ya madawa nchini,hali ambayo ilikuwa ikihatarisha maisha ya wananchi kutokana na tamaa za fedha kwa wamiliki wa maduka hayo.
Baadhi ya mambo waliobaini katika uchunguzi huo ni pamoja na wauzaji kutokuwa na elimu ya utoaji tiba,kuuza dawa moto na zisizosajiriwa kisheria badala ya dawa baridi za binadamu,kutoa mimba,kudunga sindano,kufunga vidonda na kulaza wagonjwa.
“Baada ya serikali kupitia mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la MSH tulibaini ikiukwaji mkubwa wa uendeshwaji wa maduka ya dawa baridi kutokana na kuuza dawa wasizoruhusiwa kisheria na kutoa huduma za kitabibu kinyume na maadili,hatua aliyopelekea seriakali kubuni mpango mkakati wa kuwaelimisha wamiliki na wauzaji wa maduka hayo”alisema
Katika taarifa ya mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya chakula na dawa TFDA iliyotolewa na Dk Bundara Maganga  katika mafunzo maalumu ya wauzaji wa maduka ya madawa baridi ya binadamu ambayo yanatarajiwa kupandishwa hadhi na kuwa maduka muhimu ya dawa alisema mpango huo umeonyesha mafanikio makubwa zaidi hasa katika mkoa wa Ruvuma ambako utekelezaji wake ulianza tangu februali 2002.
Aidha alisema mpango huo umetekelezwa katika mikoa 15 ya Tanzania na kuonyesha mafanikio makubwa baada ya wauzaji hao kutambua sheria na kanuni za utoaji wa sahihi wa dawa,kuelewa mbinu za magonjwa yatokeayo mara kwa mara katika jamii,huduma kwa magonjwa ya watoto,stadi za mawasiliano na elimu ya ukimwi na ushauri nasaha.
Alizitaja mikoa zilizoinufaika mafunzo hayo kuwa ni Ruvuma,kigoma,Manyara Lindi,Mbeya,Shinyanga,Pwani ,Dododma,Mara,Iringa,Singida,Tanga,Mtwara,Morogoro na rukwa huku mikoa mingine sita ikiwemo Kagera ikiendelea kupatiwa mafunzo hayo kwa kuzingatia uwezo wa seriakali.
Alisema kutokana na mpango huo wa seriakali itakuwa ni marufuku kwa mmiliki yoyote wa duka la dawa muhimu kuajiri mtumishi asiye na sifa zinazotakiwa kisheria na kwamba hatua hiyo itasaidia kuinua maendeleo ya jamii kutokana na wananchi kupata huduma yenye uhakika wa afya zao.
Mganga mkuu wa wilaya ya chato mkoa mpya wa geita ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo Dk Athanas Ngambakubi alisema mafunzo hayo ya siku 35 yatawasaidia kuongeza uelewa na mbinu sahihi za utoaji huduma kwa wagonjwa wao ukilinganisha na awali.
Dk Ngambakubi alisema kuwa iwapo dawa zikitumiwa kwa usahihi huleta matunda yaliyokusudiwa na dakatari  pamoja na  jamii,lakini kinyume chake zikitumika isivyofaa hugeuka na kuwa sumu hivyo husababisha madhara makubwa ambayo hayakukusudiwa.
Aidha alidai hatua hiyo itawasaidia kupewa vyeti vinavyotambuliwa na serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii,hatua itakayowasaidia kuongeza soko la ajira yao sanjari na kukua kwa mishahara yao ukilinganisha ha ilivyo hivi sasa.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo Ayubu Daniel na Dk Pius Ngambakubi  wameipongeza serikali kwa uanzisha mpango huo utakao saidia kuongeza ajira kwa wahitimu hao na kulejesha heshima ya taaluma ya ufamasia hasa katika maeneo ya vijijini ambako huduma za kiserikali zimekuwa ngumu kuwafikia wananchi.

No comments:

Post a Comment