Wednesday, June 6, 2012




                                             LEMA ASAMBARATISHA KWA MAGUFULI

                                   Aliye kuwa Mbunge wa Arusha Mjini Bw, Godless Lema

Na Daniel Limbe,Chato
ALIYEKUWA mbunge Jimbo la Arusha Mjini Godbress Lema (CHADEMA) amezidi kuzisambaratisha ngome za waziri wa ujenzi Dk John Magufuli baada ya makada saba wa Chama cha Mapinduzi CCM jimbo la Chato kukihama chama hicho na kujinga na Chadema,huku akionekana kushangazwa na uwezo mkubwa wa waziri huyo katika kutambua wingi wa samaki walioko majini pamoja na mimba zao, lakini ameshindwa kutatua tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa jimbo lake.
 
Akizungumza na wananchi wa jimbo la chato juzi (jana) kwenye mkutano wa hadhara Lema alimtupia lawama Dk Magufuli kushindwa kuwatumikia wananchi wake katika kutatua matatizo yanayo wakabili ikiwemo ukosefu wa maji safi na salama ambapo wananchi hao wamekuwa wakitumia maji ya yasiyofaa kwa matumizi ya binadamu kutokana na kutumiwa na mifugo na wengine kuchota maji machafu ya ziwa ambayo yamekuwa yakiwasababishia magonjwa ya kuhara.
 
Lema aliwataka wananchi wa jimbo hilo kutambua kuwa saa ya ukombozi ni sasa, na kwamba hawana budi kujiunga na Chadema kwa kuwa ndiyo chama makini chenye kutetea maslahi ya wanyonge na kupambana na ufisadi wa viongozi wa nchi hii akiwemo magufuli ambaye amejilimbikizia mali kinyume cha sheria na kushindwa kuwathamini wananchi waliomchagua kuwa mbunge.
 
“Ndugu zangu inasikitisha sana kuona chato ndiyo hii…wakati nikipita njiani kuja huku nimeshuhudia ziwa likiwa karibu kabisa na makazi yenu kiasi kwamba mbunge wenu angekuwa na nia thabiti ya kuwatumikia ninaimani wananchi wa hapa msingelikuwa masikini wa kutupwa namna hii…mimi ni mara yangu ya kwanza kufika hapa lakini kutokana na mbwembwe za Magufuli bungeni kuonyesha anafahamu aina,idadi na mimba za samaki waliomo ndani ya maji niliamini Chato inafanana na Arusha kumbe la”alisema.
 
“Nimeshuhudia majumba mengi aliyojilimbikizia magufuli…sikutarajia kwa utajiri alionao kama mngelikuwa na tatizo la maji tangu uhuru wa Tanganyika …Magufuli ameshindwa kuongoza nahii inatokana na kumpa ubunge kwa takribani miaka 20 ndiyo maana amejisahau na kuona ninyi mliomchagua hamfai, kwa maana tayari ameshalewa madaraka”alisema Lema
 
Kauli hiyo ilipelekea baadhi ya wananchama 27 wa CCM wakiwemo makada saba kukihama chama hicho na kujiunga na Chadema,hatua iliyotofasiliwa kuwa ni kuendelea kuvunjwa ngome za waziri Magufuli ambaye pia ni mbunge wa jimbo la chato kutokana na nafasi zingine za wenyeviti wa vijiji 8 kati ya 11 kutwaliwa na Chadema katika uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi zilizokuwa zimeachwa wazi na viongozi waliokuwepo awali baada ya kujihudhuru na wangine kuhama makazi yao.
 
Makada wa CCM waliokihama chama hicho ni aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji cha Mkuyuni Uhuru Selemani,aliyekuwa katibu wa vijana kata ya chato, mjumbe wa baraza kuu la vijana mkoa wa kagera,mjumbe wa kamati ya utekelezaji mkoa wa kagera na katibu wa hamasa chipukizi wilaya ya chato Masumbuko Kaitila, Lusia Kahindi,Fikiri Makoye,Samwel Mkome,Emmanuel Kayila na Vigoro Lucas ambao wote walikuwa ni wanachama wa CCM.
 
Huku akitumia kauli mbiu ya “Vua gamba vaa ngwanda, na vua ukada vaa Ukamanda”Lema aliwataka watumishi wa serikali hususani jeshi la polisi kuacha kutumia nafasi zao vibaya katika kuwanyanyasa wananchi wakiwemo viongozi wa Chadema na kwamba wanantakiwa kutenda haki pasipo kuegemea kukitumikia chama tawala kwa madai kitambo kidogo kimebaki Chadema kushika utawala wa nchi.
 
Alisema baadhi ya askari polisi wamekuwa wakitumiwa vibaya na viongozi wa chama tawala kutokana na kushinikizwa kuwapiga kwa malungu,Mabomu na kuwabambikiza kesi baadhi ya wananchi na wafuasi wa vyama vya upinzani wakiamini kuwa njia hiyo itasaidia kudidimiza kasi ya mageuzi kwa jamii hatua ambayo imekuwa ikiongeza chuki kwa wananchi dhidi ya polisi na serikali yao.
 
Aidha aliwataka wananchi kwa kushirikiana na viongozi wa Chadema kushirikiana kwa pamoja kufanya maandamano ya amani kuishinikiza serikali kuwafukuza kazi watendaji wabovu na wabadhilifu wa fedha za miradi ya maendeleo ya wilaya ya chato ambazo zimedaiwa kutafunwa bila huruma huku serikali ikishindwa kuwachukulia hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kuwaburuza mahakamani.
 
“Niwaelezeni ukweli ndugu zangu,hata maandiko yanaeleza kuwa mtu mwoga hawezi kuingia kwenye utukufu wa mungu…mnatakiwa kuwa majasiri katika kudai haki yenu ambayo mnaona inaporwa na watu wachache…ikiwezekana hata watu wachache lazima wafe kwaajili ya kusaidia walio wengi”,alisema
 
Kwa upande wake Godifrey Gwakisa alimtuhumu Dk Magufuli kwa ufisadi wa kupindukia kutokana na kuiba raslimali za nchi na kuwekeza kwa maslahi yake binafsi hatua aliyodai kuwa kiongozi huyo hafai kuwa kiongozi na anapaswa kujihudhuru haraka ili kutoa mwanaya kwa wengine wenye uchungu wa kuwatumikia wananchi badala ya kuendela kumkubatia alihali wananchi wanazidi kutesema na ugumu wa maisha kila kukicha.
 
Alisema Dk Magufuli amejilimbikizia majumba zaidi ya 100 ikiwemo ghorofa alilojenga kuishi watumishi wa shamba lake lililopo nyabirezi wilayani chato mkoa mpya wa geita,farasi kwaajili ya watumishi hao kutembelea ikiwemo kanisa alilojenga nyumbani kwao na kuliita jina la marehemu mzazi wake ambalo hata hivyo lilikataliwa na wananchi baada ya kutaka madhehebu yote kuteua muda maalumu kwaajili ya kufanya ibada zao ndani ya jengo hilo ambalo linaonekana kutumia gjharama kubwa ya fedha za walipa kodi wa Tanzania.  
 

No comments:

Post a Comment