Monday, July 16, 2012

                                              AJALI YAUA 11 NA KUJERUHI 12 GEITA

                   
                                                                                                                                               
                                                                                                                                                                       
Baadhi ya marehemu waliopata ajali leo katika kijiji cha Chibingo wilayani geita mkoani hapa wakiwa wamehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti kwenye hospitali ya wilaya ya geita
Na Daniel Limbe,Geita
WATU 11 wamekufa papo hapo na wengine 12 wamejeruhiwa vibaya baada ya magari waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso katika kijiji cha Chibingo wilayani geita mkoani geita wakati gari moja aina ya Colola likiwa katika harakati za kulivuka gari lililokuwa mbele hali iliyosababisha kutokea kwa mauti hayo.

Ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 6:30 mchana ikihusisha magari matatu  huku mawili yakiwa na abiria ambapo gari namba T 813 AZE iligongana na gari lenye namba za usajiri T 344 BPL wakati likitakka kuivuka gari yenye namba T 813  AZE aiana ya Land cluser lililo kuwa likitoka Katoro kuelekea mwanza.

Mbali na magari hayo madogo pamoja na kuwa na uwezo wa kubeba abiria watano,yamekuwa yakibeba zaidi ya watu 10 kwenye gari moja ambapo wengine hupakiwa kwenye buti kama mizigo amabpo baada ya ajari hiyo baadhi ya abiria walipoteza maisha yao papo hapo.


Mashuhuda wa ajari hiyo ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini wamedai kuwa chanzo cha ajari hiyo ni mwendo kasi wa madereva wa magari hayo almaarufu "MICHOMOKO".

Akithibitisha kuwepo kwa ajari hiyo Mkuu wa Polisi Usalama Barabarani Mkoa wa Geita John Mfinanga amesema kuwa waliokufa kwenye eneo la tukio ni watu 9 na wengine wawili walikufa wakati wakipatiwa matibabu kwenye hospitali ya Wilaya ya Geita.

Na kwamba kati ya waliokufa wanaume ni watano,wanawake watatu na watoto watatu akiwemo dereva wa moja ya magari hayo.

Aidha baadhi ya marehemu wa ajali hiyo ni pamoja na Baba na watoto wake watatu amabao ni Eliud Ngovongo (Baba) Amini aliud(mtoto),Emison Eliud(mtoto)na Sala Eliud(Mtoto) huku wengine wakiwa ni Ummy Charles,Masasila Benjamini na dereva wa moja ya magari yaliyopata ajari aliyetambulika kwa jina moja la James.

Wengine ni pamoja na Daniel Osca, na James waliofahamika kwa jina moja kila mmoja.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Omari Manzie ameika katika chumba cha kuhifadhia maiti ilipo miili ya marehemu hao na kuonmyesha kusikitishwa na ajali hiyo huku akiahidi kuwashughulikia madereva wote watakaobainika kuvunja sheria za usalama barabarani kwa kushirikiana na jeshi la polisi.

Baadhi ya wananchi aakiwemo Waziri Joseph wamedai kushangazwa na wingi wa majeruhi hao hasa ikizingatiwa kuwa idadi ya maiti na majeruhi ikikusanywa inafikia abiria wa gari kubwa na kuiomba serikali kuingilia kati suala la madereva kujaza abiria kupita kiasi.

No comments:

Post a Comment